• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko/Mrejesho |
Singida Municipal Council
Singida Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Elimu Msingi na Awali
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango, na Uratibu
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
    • Units
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Sheria na Usalama
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Misitu na Maliasili
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Maziwa
      • Mawe
      • Maeneo ya Kihistoria
    • Kilimo
    • Umeme wa Jua na Upepo
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Usafi wa Mazingira
    • Ukusanyaji wa Mapato
    • Mikopo ya Wanawake, Vijana na Walemavu
    • Kituo cha Biashara
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipangomiji,Mazingira, na Ujenzi
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Time Table
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/MwenyeKiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Miongozo ya Kilimo
    • Policy
    • Fomu
    • Taarifa Ya Utekelezaji
    • Jarida
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Sheria
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa Za Kifedha
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADIWANI MANISPAA YA SINGIDA WATAKIWA KUWA KIELELEZO CHA MFUKO WA AFYA YA JAMII - iCHF

Posted on: September 7th, 2022

Wananchi Mkoa wa Singida, wametakiwa  kujiunga na Mfuko wa Bima ya afya iliyoboreshwa (iCHF), ili kuweza kupatiwa huduma bora za matibabu kupitia vituo vya afya na zahanati vilivyojengwa/ kukamilishwa  na serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Joseph Serukamba, alitoa agizo hilo wakati akizungumza na madiwani, watendaji wa Kata na wakuu wa idara na vitengo kupitia Mkutano wa Baraza la Madiwani Manispaa ya Singida, uliofanyika kwenye ukumbi wa Maktaba, katika shule ya Sekondari Mwenge.

Aidha Serukamba amesema Madiwani kama viongozi wawakilishi wa wananchi wanapaswa kuonesha mfano kwa  kuziunganisha Kaya zao katika mfuko wa  afya ya jamii (CHF), ili baadaye zinufaike na huduma bora za matibabu pindi  mwanafamilia anapougua, hali itakayookoa gharama kubwa za matibabu.

“Serikali yetu inayoongozwa na Rais mchapa kazi, mama Samia Suluhu Hassan, imefanya kazi kubwa…ametumia fedha nyingi kujenga zahanati kila Kijiji, vituo vya afya kila Kata na hospitali kwa wilaya zote nchini, sasa lazima tumuunge mkono kwa kuhamasisha wananchi kujiunga na Bima ya afya…,” alisisitiza Serukamba.

Kuhusu ushirikiano baina ya watendaji, wataalamu na madiwani katika Manispaa ya Singida, Mkuu wa Mkoa amesema kuwa hategemei kuona ushirikiano huo ukilegalega kutokana na kila upande kushindwa kutekeleza vema majukumu yake. Na kuwataka kila mmoja kutekeleza majukumu yake kulingana na nafasi anayotumika ili kuondoa migongano isiyokuwa ya lazima, lengo likiwa ni kuiletea manispaa ya Singida maendeleo.

Aliwataka wataalamu na watendaji wa Manispaa ya Singida, kutumia weledi katika kuongeza mapato ya ndani kupitia vyanzo mbalimbali kwa kuwa na mkakati madhubiti wa ukusanyaji mapato na uibuaji wa vyanzo vipya vyenye tija.

Serukamaba pia amesisitiza suala la kuuweka mji kwenye hali ya usafi ili uwe nadhifu na kuvutia wageni wanaoingia na kutoka Pamoja afya za wananchi wa Manispaa ya Singida ambao ndiyo kitovu cha Mkoa wa Singida.

“Mheshimiwa Meya, naomba sana muwe na mkakati wa kuongeza mapato, kwa kupitia vyanzo vya mapato, na muwe wabunifu katika kupata vyanzo vipya ambavyo vitainua mapato yenu, kuliko mlivyo sasa asilimia 90,”amefafanua.

Kuhusu suala la hoja za ukaguzi, Serukamba alisema hatarajii kuona hoja za ukaguzi zikiongezeka  na kwamba  suala hilo linapaswa kudhibitiwa mapema na mkaguzi wa ndani ili kuepuka kuzalishwa kwa hoja za Ukaguzi na kumtaka Mkaguzi wa Ndani kuwajibuka ipasavyo katika majukumu yake.

“Kuzalishwa kwa hoja nyingi za ukaguzi tafsiri yake ni uzembe katika kusimamia na kufuata sheria za fedha…” amesema Serukamba

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu amemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa kwa nasaha zake mbele ya mkutano huo wa Baraza la Madiwani, na kumhakikishia kuwa maagizo aliyotoa yatasimamiwa na kutekelezwa kwa maslahi ya wananchi wa Manispaa ya Singida.

Mkuu wa Mkoa wa Singida amefanya  ziara hiyo katika Manispaa ya Singida kwa lengo la kujitambulisha kwa waheshimiwa madiwani pamoja na watumishi kufuatia kuteuliwa kwake na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan, kwa nafasi ya  Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ March 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO DIRISHA LA ROBO YA TATU January 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU MWENYE ULEMAVU KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SINGIDA October 02, 2024
  • MATOKEO YA VITENDO KWA DEREVA October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari za hivi Punde

  • KONGOLE MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUPEWA TUZO MAALUM YA HESHIMA NA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

    May 31, 2025
  • Meya atoa onyo kwa wasiotunza mazingira Manispaa ya Singida

    May 31, 2025
  • MKURUGENZI WA MANISPAA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAUGUZI MKOA WA SINGIDA

    May 30, 2025
  • WANANCHI 35 WAFANYIWA UPASUAJI WA MTOTO WA JICHO SINGIDA

    May 29, 2025
  • Tazama Zote

Video

UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST HADI TAREHE 02 JUNI 2023 - MANISPAA YA SINGIDA
Video Zaidi

Viunganisho vinavyohusiana

  • Press Release

Kurasa za Karibu

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karume Road Street

    Sanduku la Posta: P.O BOX 236,Singida

    Telephone: +255 26 250 2179/236

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: md.singidamc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

© 2018 Halmashauri ya Manispaa ya Singida.Haki zote zimehifadhiwa.