• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko/Mrejesho |
Singida Municipal Council
Singida Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Elimu Msingi na Awali
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango, na Uratibu
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
    • Units
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Sheria na Usalama
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Misitu na Maliasili
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Maziwa
      • Mawe
      • Maeneo ya Kihistoria
    • Kilimo
    • Umeme wa Jua na Upepo
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Usafi wa Mazingira
    • Ukusanyaji wa Mapato
    • Mikopo ya Wanawake, Vijana na Walemavu
    • Kituo cha Biashara
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipangomiji,Mazingira, na Ujenzi
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Time Table
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/MwenyeKiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Miongozo ya Kilimo
    • Policy
    • Fomu
    • Taarifa Ya Utekelezaji
    • Jarida
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Sheria
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa Za Kifedha
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERUKAMBA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WATENDAJI ILI KUKABILIANA NA UGONJWA WA MLIPUKO

Posted on: November 7th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewaagiza Viongozi na Watendaji Mkoani humo kuhakikisha kaya zote zinakuwa na vyoo bora na kuchukua hatua kali kwa mujibu wa sheria dhidi ya kaya ambazo hazina vyoo ili kukabiliana na ugonjwa wa mlipuko wa kuharisha na kutapika.


Akizungumza leo tarehe (7 Novemba, 2023) kwenye kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi cha Mkoa kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, Serukamba amesema maradhi hayo husababishwa na mazingira ya uchafu hivyo jamii inapaswa kuhakikisha mazingira yote yanayowazunguka yanakuwa safi kwa lengo la kudhibiti magonjwa ya mlipuko hasa Kipindupindu ili kisiwepo kabisa Mkoani Singida.


Aidha, Serukamba amewasisitiza Wakuu wa Wilaya wote Mkoani humo kuhakikisha maeneo yote ya kaya, taasisi za umma, mashirika ya dini, masoko, stendi za mabasi, mashuleni, kwenye nyumba za ibada na mikusanyiko rasmi na isio rasmi kuwa na vifaa vya kunawia mikono, maji safi na sabuni ili kujikinga na maradhi hayo.


Amewasisitiza Wakuu hao wa Wilaya kwa kushirikiana na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha maeneo yote ya kupikia na kuuzia vyakula yanakaguliwa na wataalamu wa Afya ili kuwa safi muda wote. Aidha kila Halmashauri ifanye kikao cha kamati ya Afya ya Msingi pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo.


Hata hivyo Serukamba, amewaagiza Wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (SUWASA), Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa Singida (RUWASA) pamoja na Mkurugenzi wa Bodi Bonde la Kati kuhakikisha wanachukuwa sampuli za maji na kutibu visima vifupi, virefu na kusambaza maji safi na salama kwa watumiaji maji hayo ili kujikinga na ugonjwa huo wa kuharisha na kutapika.


Katika hatua nyingine, amewahimiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa huo kuhakikisha maeneo yote ya minada na masoko yanakuwa na vyoo bora ili kuepuka kusambaa kwa ugonjwa huo wa mlipuko wa kuharisha na kutapika hasa katika Mkoa wa Singida.


Mkuu wa Mkoa huyo amewaagiza Waganga Wakuu wa kila Halmashauri kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi juu ya kukabiliana na magonjwa ya kuharisha na kutapika.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ March 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO DIRISHA LA ROBO YA TATU January 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU MWENYE ULEMAVU KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SINGIDA October 02, 2024
  • MATOKEO YA VITENDO KWA DEREVA October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari za hivi Punde

  • INEC YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI

    May 14, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA VYA SIASA WALA KIAPO CHA UTII

    May 12, 2025
  • MANISPAA YA SINGIDA YATAKIWA KUPIMA MAENEO KABLA YA KUTEKELEZA MIRADI

    May 09, 2025
  • “PONGEZI KWAKO, RC HALIMA DENDEGO”

    May 09, 2025
  • Tazama Zote

Video

UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST HADI TAREHE 02 JUNI 2023 - MANISPAA YA SINGIDA
Video Zaidi

Viunganisho vinavyohusiana

  • Press Release

Kurasa za Karibu

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karume Road Street

    Sanduku la Posta: P.O BOX 236,Singida

    Telephone: +255 26 250 2179/236

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: md.singidamc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

© 2018 Halmashauri ya Manispaa ya Singida.Haki zote zimehifadhiwa.