• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko/Mrejesho |
Singida Municipal Council
Singida Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Elimu Msingi na Awali
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango, na Uratibu
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
    • Units
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Sheria na Usalama
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Misitu na Maliasili
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Maziwa
      • Mawe
      • Maeneo ya Kihistoria
    • Kilimo
    • Umeme wa Jua na Upepo
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Usafi wa Mazingira
    • Ukusanyaji wa Mapato
    • Mikopo ya Wanawake, Vijana na Walemavu
    • Kituo cha Biashara
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipangomiji,Mazingira, na Ujenzi
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Time Table
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/MwenyeKiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Miongozo ya Kilimo
    • Policy
    • Fomu
    • Taarifa Ya Utekelezaji
    • Jarida
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Sheria
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa Za Kifedha
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA SINGIDA ASIKILIZA KERO ZA WANANCHI WA MANISPAA YA SINGIDA

Posted on: January 17th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, ameagiza Wataalamu na Viongozi wa Manispaa ya Singida kuwa karibu zaidi na Wananchi wao, ili kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazoikabili jamii ya Halmashauri hiyo.

Serukamba ametoa maagizo hayo, baada ya kusikiliza kero za Wananchi wa Manispaa ya Singida, kwenye kikao kilichofanyika katika ukumbi wa jengo la ofisi Mkuu wa Mkoa na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.

Kwenye Kikao hicho, licha ya idadi kubwa ya Wananchi kujitokeza, pia Watendaji wa Kata, Wakuu wa divisheni na vitengo wa Manispaa ya Singida, walishiriki ili kujibu hoja za lazima, zilizowasilishwa na Wananchi.

“Utatuzi wa kero za Wananchi ni jambo linaloleta matumaini kwao pia ni  utekelezaji wa ilani ya CCM, tuendelee na utaratibu huu…kwa kweli ndiyo kazi yetu, tusisubiri hadi waje wakubwa, ndipo tutatue kero zao,” alisema Serukamba.

Alifafanua kuwa, baadhi ya kero zilizowasilishwa hazihitaji fedha wala nguvu kubwa kuweza kuzitatua, bali ni majibu mazuri, yenye kuakisi matumaini, katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto hizo zinazoikabili jamii.

Baadhi ya kero zilizotawala katika kikao hicho ni malalamiko dhidi ya idara ya ardhi kero 15, madeni ya wazabuni, afya, TASAF na usafi na mazingira.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Mkoa, aliwataka Wataalamu, wakiwemo watendaji wa Kata na ofisi ya Mkurugenzi, kukutana na Wananchi mara kwa mara, badala ya kusubiri viongozi wakubwa wanapokuwa katika ziara zao.

Pamoja nayo Mkuu huyo wa mkoa amesisitiza suala la utoaji elimu kwa wananchi ikiwa ni moja ya mkakati wa kupunguza kero kwa wananchi  ambapo alisema, wananchi wakielimishwa vyema changamoto ama matatizo yao yatamalizwa katika ngazi ya Kata na Ofisi ya Mkurugenzi

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida, Jeshi Godfrey Lupembe, alibainisha kuwa, kupitia kikao hicho wataalamu wameweza kujifunza, kutokana na kero zilizowasilishwa na Wananchi.

“Matatizo haya tunayoyaona hapa, kama kungekuwa na vikao vya kisheria ngazi ya Kata, hapa leo mapungufu yasingejitokeza…sisi watumishi wako leo tumeona kwa vitendo unavyofundisha, tunakuahidi yote uliyoelekeza tutayafanyia kazi,” alisema Jeshi.

Mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba, amepanga ratiba ya kusikiliza kero kwa wananchi wa mkoa wake kila mwezi, akianza katika Manispaa ya Singida, kwa kufungua mlango huo.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ March 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO DIRISHA LA ROBO YA TATU January 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU MWENYE ULEMAVU KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SINGIDA October 02, 2024
  • MATOKEO YA VITENDO KWA DEREVA October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari za hivi Punde

  • MAENDELEO YA UJENZI WA SHULE YA AMALI MKOA WA SINGIDA

    May 21, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU PILI

    May 20, 2025
  • MIAKA MINNE YA MHE. DKT SAMIA SULUHU HASSAN ASANTE KWA KUBORESHA MAZINGIRA YA WAFANYAKAZI

    May 20, 2025
  • "UPATIKANAJI WA HAKI KUONGEZA IMANI KWA WANANCHI"

    May 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST HADI TAREHE 02 JUNI 2023 - MANISPAA YA SINGIDA
Video Zaidi

Viunganisho vinavyohusiana

  • Press Release

Kurasa za Karibu

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karume Road Street

    Sanduku la Posta: P.O BOX 236,Singida

    Telephone: +255 26 250 2179/236

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: md.singidamc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

© 2018 Halmashauri ya Manispaa ya Singida.Haki zote zimehifadhiwa.