• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko/Mrejesho |
Singida Municipal Council
Singida Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Elimu Msingi na Awali
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango, na Uratibu
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
    • Units
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Sheria na Usalama
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Misitu na Maliasili
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Maziwa
      • Mawe
      • Maeneo ya Kihistoria
    • Kilimo
    • Umeme wa Jua na Upepo
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Usafi wa Mazingira
    • Ukusanyaji wa Mapato
    • Mikopo ya Wanawake, Vijana na Walemavu
    • Kituo cha Biashara
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipangomiji,Mazingira, na Ujenzi
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Time Table
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/MwenyeKiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Miongozo ya Kilimo
    • Policy
    • Fomu
    • Taarifa Ya Utekelezaji
    • Jarida
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Sheria
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa Za Kifedha
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC: SINGIDA AAGIZA TAKUKURU KUSHIRIKIANA NA VYAMA VYA WAFANYAKAZI KUONDOA RUSHWA ZA AINA ZOTE KATIKA HALMASHAURI NA TAASISI ZA UMMA

Posted on: May 1st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr. Binirith Mahenge ameiagiza Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kushirikiana na vyama vya wafanyakazi kuhakikisha rushwa za aina zote zinakomeshwa katika Halmashauri na Taasisi mbalimbali za Umma.

Dr. Mahenge ameyasema hayo katika maadhimisho ya Sherehe ya siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi) zilizoadhimishwa kimkoa katika uwanja wa Namfua Mkoani Singida.

Alisema amefarijika kusikia katika risala iliyosomwa na Mratibu wa TUCTA mkoa kuwa rushwa ya ngono imepungua kwa kiasi kikubwa katika Taasisi za umma hivyo kutoa agizo kwa TAKUKURU kushirikiana na vyama vya wafanyakazi kuondoa rushwa zote makazini.

Aidha amesema waajiri na waajiriwa kwa Pamoja wanapaswa kuzingatia sheria Na. 6 ya mwaka 2004 ili kuhakikisha uadilifu na haki vinazingatiwa katika utoaji huduma katika taasisi zote.

Kuhusu suala la waajiri kuchelewesha michango ya Watumishi katika mifuko ya hifadhi ya ya Jamii, Mkuu wa Mkoa ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi ,ameiagiza TUCTA kuwasilisha kwake orodha ya waajiri wanaochelewesha michango ya waajiriwa sambamba na madai ya waajiriwa ili aweze kushughulikia nao.

Amewaasa Watumishi kujenga utamaduni wa kutembelea mifuko ya hifadhi ili kujua taarifa za michango yao badala ya kusubiri muda wa kustaafu unapofika ili kuepuka usumbufu.

Pamoja na masuala mengine ya Maendeleo Dr. Mahenge ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa miradi ya Maendeleo katika nyanja za elimu, afya, barabara na TASAF ambapo kwa mkoa waSingida kiasi cha takribani Tshs. Bilioni 232 zimepokelewa kwa ajili ya miradi ya Maendeleo

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida Bi. Doroth Mwaluko amewapongeza watumishi kwa kutekeleza majukumu yao vizuri na kuwataka kufuata taratibu za kiutumishi kwa umakini zaidi ili kuhakikisha shughuli za maendeleo na huduma kwa wananchi hazikwami.

“nimeona mnacheza vizuri mziki wa kwaito kwa kufuata step barabara, vivyo hivyo mfuate step za kiutumishi katika utekelezaji wa majumu yenu” alisisitiza Bi. Mwaluko.

Mratibu wa wa TUCTA Bi. Susan Shashi kupitia risala amepongeza watumishi wote kwa utekelezaji mzuri wa majukumu na hasa Wakurugenzi waliotoa kipaumbele kwa mabaraza ya wafanyakazi kufanyika katika kipindi cha bajeti na tahmini ya utekelezaji wa shughuli za Maendeleo kwani yameleta ufanisi mkubwa katika utekelezaji shughuli za Maendeleo.

Aidha Bi Suzan amewataka Wakurugenzi kuhakikisha wanalipa kwa wakati fedha za uhamisho wa watumishi pindi unapofanyika ili kuepuka kuleta usumbufu kwa mtumishi/Watumishi waliohamishwa. Pamoja na malipo ya uhamisho ametaja masuala mengine ambayo yanaleta usumbufu kwa Watumishi kuwa ni Pamoja na madai mbalimbali ya shahiki zao na adhabu zinazotolewa kwa Watumishi bila sababu za msingi.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa dini mbalimbali katika mkoa wa Singida Mwenyekiti wa Dini Mbalimbali ambaye pia ni Diwani wa kata ya Misuna Mhe. Hamis Momahed Kisuke amewataka watumishi kuwa waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuepuka dhuluma ili haki itendeke na amani itawale.

“Ndugu zangu watumishi jitahidini kuepuka dhuluma ili haki itendeke kwani bila haki amani inatoweka na hivyo migogoro kuibuka”, aliasa Mhe. Kisuke

Watumishi wa Idara ya Afya katika Manispaa ya Singida wakipita kwa madaha mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr. Binirith Mahenge katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani


Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Ndg. Kulaga Kanyanga ( Mwenye Miwani) akisikiliza kwa makini risala iliyosomwa na Mratibu wa TUCTA mkoa wa Singida

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ March 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO DIRISHA LA ROBO YA TATU January 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU MWENYE ULEMAVU KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SINGIDA October 02, 2024
  • MATOKEO YA VITENDO KWA DEREVA October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari za hivi Punde

  • MAENDELEO YA UJENZI WA SHULE YA AMALI MKOA WA SINGIDA

    May 21, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU PILI

    May 20, 2025
  • MIAKA MINNE YA MHE. DKT SAMIA SULUHU HASSAN ASANTE KWA KUBORESHA MAZINGIRA YA WAFANYAKAZI

    May 20, 2025
  • "UPATIKANAJI WA HAKI KUONGEZA IMANI KWA WANANCHI"

    May 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST HADI TAREHE 02 JUNI 2023 - MANISPAA YA SINGIDA
Video Zaidi

Viunganisho vinavyohusiana

  • Press Release

Kurasa za Karibu

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karume Road Street

    Sanduku la Posta: P.O BOX 236,Singida

    Telephone: +255 26 250 2179/236

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: md.singidamc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

© 2018 Halmashauri ya Manispaa ya Singida.Haki zote zimehifadhiwa.