• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko/Mrejesho |
Singida Municipal Council
Singida Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Elimu Msingi na Awali
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango, na Uratibu
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
    • Units
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Sheria na Usalama
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Misitu na Maliasili
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Maziwa
      • Mawe
      • Maeneo ya Kihistoria
    • Kilimo
    • Umeme wa Jua na Upepo
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Usafi wa Mazingira
    • Ukusanyaji wa Mapato
    • Mikopo ya Wanawake, Vijana na Walemavu
    • Kituo cha Biashara
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipangomiji,Mazingira, na Ujenzi
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Time Table
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/MwenyeKiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Miongozo ya Kilimo
    • Policy
    • Fomu
    • Taarifa Ya Utekelezaji
    • Jarida
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Sheria
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa Za Kifedha
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI MANISPAA YA SINGIDA WAASWA KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA

Posted on: June 14th, 2022

Watumishi Manispaa ya Singida wametakiwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kuwajibika ipasavyo kwa wananchi ambao wapewa dhamana ya kuwahudumia kupitia utaalamu wao.

Hayo yamesemwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Mhe. Yagi Kiaratu (13.06.2022) wakati akizungumza na watumishi wa kata tatu za Ipembe, Majengo na Misuna katika kikao kazi kilichoandaliwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo ikiwa ni utaratibu uliowekwa wa kuzungumza na watumishi katika kata.

Mhe. Yagi ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Majengo alisema vikao kama hivi ni Sehemu ya kukumbushana wajibu wa kiutumishi ambao kwa namna moja ama nyingine watumishi wamekuwa wakijisahau ama kurithi masuala ya kiutendaji ambayo ni kinyume na taratibu za kiutumishi kutoka kwa watangulizi wao hivyo kuathiri utoaji huduma kwa Jamii.

“Forum kama hii inawakumbusha kuwajibika kwa kada mnayoitumikia pia kwa Jamii inayowazunguka ili iendelee kujenga imani na nyie kwa uadilifu unaouonesha” alisisitiza Mhe. Yagi

Alisema elimu nzuri na utaalamu walionao Watumishi hauna faida kama hawataweza kuionesha kupitia huduma bora kwa Jamii na mahusiano mazuri baina yao na Jamii inayowazunguka na kuongeza kuwa ni jukumu la watumishi kujenga taswira nzuri ya Serikali kupitia uwajibikaji wao.

“Tumieni nafasi hii kuzungumzia changamoto zinazowakabili ambazo kwa namna moja ama nyingine zinaathiri utendaji kazi wenu” alisisitiza.

Aidha amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa pamoja na masuala mengine kuhakikisha usalama wa watumishi unakuwepo wawapo kazini hii ikiwa ni pamoja na mazingira wanayofanyia kazi na kutatua changamoto zinazowakabili kwa wakati.

Mhe. Yagi amesema ofisi ya Mkurugenzi ina wajibu wa kujenga mahusiano mazuri na vyama vya wafanyakazi ili kuweza kushirikiana pamoja katika kutatua migogoro ya wafanyakazi na changamoto zinazowakabili kabla ya kupelekana mbele ya sheria.

Ametoa rai kwa Watumishi kuwajibika ili kuleta matokeo chanya na kuongeza kuwa ni aibu kwa mtumishi kulalamikia Serikali wakati hana alichoitendea Serikali ambacho kinapimika na kusema kuwa haki ni lazima iendane na wajibu.

“kabla hujailalamikia Serikali hebu jiulize wewe umeitendea nini Serikali”, alisistiza mhe. Yagi

Alisema watumishi wa Serikali popote walipo ni jeshi la Mhe. Rais na wanawajibika kuitendea haki Serikali kwa kutoa huduma iliyo bora kwa wananchi na kuitendea haki nafasi yake aliyopewa kama mtumishi wa umma.

“Watumishi mnauza huduma hivyo wateja wenu ambao ni Jamii lazima waridhike na huduma mnazotoa kupitia lugha nzuri, uwajibikaji bora na mahusiano mazuri” aliasa Mhe. Yagi

Mkakati wa Manispaa ya Singida wa kuzungumza na watumishi wa kata ni endelevu  ili kuiwezezesha Halmashauri kubaini changamoto zinazowakabili watumishi wake na hivyo kuzitatua kwa wakati na kuboresha utendaji kazi wa watumishi.

Matangazo

  • TANZANIA CITIES TRANSFORMING INFRASTRUCTURE AND COMPETITIVENESS (TACTIC) PROJECT IDA CREDIT NO. 7151-TZ March 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO DIRISHA LA ROBO YA TATU January 10, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU MWENYE ULEMAVU KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SINGIDA October 02, 2024
  • MATOKEO YA VITENDO KWA DEREVA October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari za hivi Punde

  • MAENDELEO YA UJENZI WA SHULE YA AMALI MKOA WA SINGIDA

    May 21, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU PILI

    May 20, 2025
  • MIAKA MINNE YA MHE. DKT SAMIA SULUHU HASSAN ASANTE KWA KUBORESHA MAZINGIRA YA WAFANYAKAZI

    May 20, 2025
  • "UPATIKANAJI WA HAKI KUONGEZA IMANI KWA WANANCHI"

    May 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST HADI TAREHE 02 JUNI 2023 - MANISPAA YA SINGIDA
Video Zaidi

Viunganisho vinavyohusiana

  • Press Release

Kurasa za Karibu

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karume Road Street

    Sanduku la Posta: P.O BOX 236,Singida

    Telephone: +255 26 250 2179/236

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: md.singidamc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

© 2018 Halmashauri ya Manispaa ya Singida.Haki zote zimehifadhiwa.