• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko/Mrejesho |
Singida Municipal Council
Singida Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Elimu Msingi na Awali
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango, na Uratibu
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
    • Units
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Sheria na Usalama
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Misitu na Maliasili
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Maziwa
      • Mawe
      • Maeneo ya Kihistoria
    • Kilimo
    • Umeme wa Jua na Upepo
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Usafi wa Mazingira
    • Ukusanyaji wa Mapato
    • Mikopo ya Wanawake, Vijana na Walemavu
    • Kituo cha Biashara
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipangomiji,Mazingira, na Ujenzi
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Time Table
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/MwenyeKiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Miongozo ya Kilimo
    • Policy
    • Fomu
    • Taarifa Ya Utekelezaji
    • Jarida
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Sheria
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa Za Kifedha
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

USHIRIKIANO WA WALIMU NA WAZAZI (UWaWa) UMELETA MAFANIKIO KATIKA SHULE NA KWENYE JAMII

Posted on: February 28th, 2023

Washiriki wa mafunzo ya uboreshaji shughuli za maendeleo ya elimu Leo tarehe 28February, 2023, wameeleza kuwepo kwa mafanikio makubwa tangu mafunzo kuhusu ushirikiano wa walimu na wazazi kupitia programu  ya Shule Bora kuanzishwa katika shule za Msingi Manispaa ya Singida.

Akitoa ushuhuda wa namna UWaWa ulivyoweza kuleta manufaa katika shule na jamii kwa ujumla, Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mtamaa, Bryson Zera, amesema, kupitia ushirikiano huo wazazi walikubaliana katika kikao ya kwamba kwa kila mtoto atakayekuwa mtoro mzazi atawajibika kulipa faini ya Tshs, 1,000.

Amesema kutokana na makubaliano hayo, wazazi wengi wamewajibika kuhakikisha watoto wanakwenda shule wakati walimu nao wanahakakikisha wanasimamia mahudhurio vyema ili kuwabaini watoro, hali ambayo kwa mujibu wa mwalimu mkuu huyo imepunguza  hali ya utoro shuleni hapo.

Naye Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi mwankoko amesema kupitia UWaWa jamii imehamasika na kuweza kuchangia ujenzi wa msingi wa chumba kimoja cha darasa shule msingi Mwankoko, msingi wa vyumba 02 vya madarasa na ofisi katika shule ya msingi Makungu. Na kwamba si hayo tu bali pia kwa upande wa taaluma, wazazi kupitia UWaWa, wameweza  kuchangia gharama za uendeshaji wa mitihani ya majaribio kila mwisho wa wiki shuleni hapo.

Mwalimu Hashimu Aladin wa Shule ya Msingi Minga amesema katika shule yake pamekuwa na vitendo vya udhalilishaji wanafunzi hasa watoto wadogo kutokana na uwepo wa mazingira ya vichaka na nyumba ambazo hazijakamilika ( maboma) ambayo yamepakana na shule hiyo.

“ Vitendo vya ulawiti vimekuwa vikifanyika kwa wanafunzi hasa wale wadogo…… UWaWa imeleta mabadiliko… ushirikiano baina ya wazazi na walimu katika kutatua tatizo hili umekuwa ni mkubwa na hivyo kupungua kwa vitendo  vya udhalilishaji watoto”, amesema Mwl. Aladin.

Pamoja naye Mwalimu Mwanamwema Nkhua wa Shule ya msingi Mughanga amesema UWaWa umeleta mwamko mpya kwa wazazi wa kushiriki mikutano ya wazazi na kutoa maoni  tofauti na hapo awali hivyo kuleta wepesi katika kutatua changamoto za wanafunzi za kitaaluma na kimaadili shuleni hapo.

Mwalimu Emmanuel Kimweri wa Unyakumi Shule ya Msingi amesema, UWaWa imekuwa ni daraja kubwa kati ya walimu na wazazi na kwamba kupitia ushirikiano huo, waliweza kuwarejesha wanafunzi watoro na kuendelea na masomo.

“ hatukutumia nguvu kwani wazazi walioko kwenye kamati wanawajua vyema wazazi wa watoto husika hivyo ilikuwa rahisi kuwafikia na kusema nao na mapokeo yakawa mazuri kwani watoto walirudi kuendelea na masomo”, amesema Mwalimu Kimwezi.

Mkufunzi wa mafunzo hayo ngazi ya Halmashauri ya Manispaa, Bi. Salome Kyomo, amesema kwa shule yoyote ile,  ili iweze kufanya vizuri hapana budi kuwepo ushirikiano baina ya walimu na wazazi.

Amesema serikali kwa kuliona hilo, inatoa mafunzo ya UWaWa kwa walimu, wenyeviti wa kamati za shule, na maafisa elimu Kata ili kuweza kuwaimarisha na hivyo kuweza kusimamia shule zao ipasavyo, kwa kuhakikisha mwanafunzi anasoma katika mazingira salama na mazuri kwa kujifunza.

“ UWaWa imeenda mbali zaidi… kamati za shule zipo … UWaWa imejikita zaidi kwenye madarasa kuanzia awali mpaka la saba….”amesema Kyomo.

Jumla ya walimu wakuu 53, wenyeviti wa kamati za shule 53, maafisa elimu Kata 18 na wakufunzi 4 wameshiriki katika mafunzo hayo katika Manispaa ya Singida.

Mwisho

Matangazo

  • MAPITIO YA BAJETI 2022/2023 February 21, 2023
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA MANISPAA YA SINGIDA KWA SHULE 2021 November 15, 2021
  • KARIBU UWEKEZE KATIKA MANISPAA YA SINGIDA November 15, 2022
  • TATHMINI YA MATOKEO YA MITIHANI YA DARASA LA SABA 2022 KI- SHULE December 23, 2022
  • Tazama Zote

Habari za hivi Punde

  • KAYA 5,396 MANISPAA YA SINGIDA ZIMENUFAIKA NA MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII (TASAF) DIRISHA LA SEPTEMBA - OKTOBA, 2023

    March 22, 2023
  • BOT YATOA ELIMU YA FEDHA BANDIA KWA WAFANYABIASHARA WA SOKO LA KIMATAIFA LA VITUNGUU, MISUNA MANISPAA YA SINGIDA

    March 20, 2023
  • TUME YA UTUMISHI YA WALIMU SINGIDA YAWATAKA WALIMU KUZINGATIA SHERIA,KANUNI NA MIONGOZO INAYOTOLEWA NA SERIKALI

    March 20, 2023
  • MIAKA MIWILI YA DHAHABU YA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN YALETA MAPINDUZI YA MAENDELEO SINGIDA

    March 18, 2023
  • Tazama Zote

Video

Waziri Jafo atoa maagizo mazito kwa ma-RAS, ma-DED, Wakuu wa idara na maasifa mawasiliano serikalini
Video Zaidi

Viunganisho vinavyohusiana

  • Press Release

Kurasa za Karibu

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karume Road Street

    Sanduku la Posta: P.O BOX 236,Singida

    Telephone: +255 26 250 2179/236

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: md.singidamc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

© 2018 Halmashauri ya Manispaa ya Singida.Haki zote zimehifadhiwa.